Magufuli Nomaaa..Awakilishwa Kwenye Kikao Kingine cha Kimataifa Nnje ya Nchi....!!!


Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa amekutana na Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda wakati akiwa uwanja wa ndege wa Julius Nyerere akielekea Port Louis, Mauritius.

 Waziri Mkuu, anakwenda Mauritius kumwakilisha Rais John Magufuli, katika uzinduzi wa Jukwaa la Uchumi la Afrika(The inaugural session of The African Economic Platform).

Mauritius inakuwa mwenyeji wa mkutano huo utakaofanyika kuanzia Machi 20 hadi 22 katika hoteli ya Turtle Bay, jijini Balaclava.

 Waziri Mkuu wa Mauritius, Pravid Jugnauth atafungua mkutano huo ambao pia utahudhuriwa na viongozi wakuu wa kisiasa wa Afrika, wafanyabiashara, vyuo vikuu, sekta binafsi na wasomi.

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad