Mapenzi Haya Khaa....! Nimeenda Kwetu Kujifungua Kurudi Namkuta na Mwanamke Mwingine..!!!


Naomba ushauri, 

Nina mume nipo naye mwaka wa nne na tumepata mtoto mmoja wa kiume, lakini cha kushangaza nilipojifungua nimeenda kwetu kurudi nakuta anamwanamke mwingine na bila kujua kumbe kabla yangu anamtoto mwingine. 

Nilipomuuliza alisema walishindwana kisa dini, baada ya hapo ndo kanipata mimi lakini baada ya kurudi nyumbani naona anamwanamke mwingine tena kamzidi umri, nikimuuliza ananipiga, kumbe yule mwanamke anamimba na ninavyoongea sasahivi ameshajifungua mtoto.

Nilipojua inauma sana na kumpeleka kwa ndugu zake akatubu kweli mtoto wake akasema alipitiwa lakini cha ajabu bado anaendelea na huyo mwanamke
ukimuuliza anasema mtoto anaumwa nilienda kumwona.

Huwa ananiaga anaenda kanisani kumbe anaenda kwa huyo mwanamke alafu anataka mtoto akikuwa aniletee mimi wote nyumbani. Jamani naumia sana na sijawahi kumsaliti na natimiza kazi zangu zote kama mke.

Naombeni ushauri jamani maana hali tete.

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad