Noma Sana..Nay wa Mitego Amkaushia Rais Magufuli Pamoja na Kuachiliwa Huru kwa Amri Yake,


Msanii wa muziki wa hip hop Nay wa Mitego amefunguka mengi mbele ya waandishi wa habari muda mchache baada ya kuachiwa na jeshi la polisi.

Rapa huyo alishikiliwa na jeshi hilo kwa siku mbili baada ya wimbo wake mpya ‘Wapo’ kuonekana hauna maadili.

Akiongea na waandishi wa habari baada ya kutoka kituo cha polisi alipokuwa akishiliwa, Nay ameishukuru serikali pamoja na wadau mbalimbali ambao walikuwa wanampambania.

“Nawashukuru sana watu wa media, wanasheria wangu ndugu jamaa na marafiki kwa upendo waliouonyesha kwangu. Pia naishukuru serikali kwa hichi walichokifanya, sasa hivi sina kubwa la kuongea wimbo umeruhusiwa nashukuru na nimefurahi kusikia hivyo,” alisema Nay wa Mitego.

Rapa huyo amesema kwa sasa anajipanga kufanya maandalizi ya kuandaa video kwajili ya wimbo huo.

Katika taarifa iliyotolewa mapema leo na Rais Magufuli alisema wimbo huo ni mzuri lakini aongezee changamoto nyingine zilizopo kwenye jamii.

Post a Comment

2 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.
  1. UMESHAPATA KIKI

    ReplyDelete
  2. Theme ya rap music ni kuongea yaliyopo ktk jamii sasa TZ walipanick nini mpaka kuweka mtu ndani?

    Go Nay!!

    ReplyDelete

Top Post Ad

Below Post Ad