Ridhiwani Kikwete - Baba Aliamua Kuficha Hofu Yake Baada ya Kutajwa Kwenye List ya Wanaouza Madawa ya Kulevya Ili Kunitia Nguvu ...!!!


Baada ya kuitwa kuhojiwa kuhusu tuhuma za kuhusika na biashara ya dawa za kulevya, Mbunge wa Chalinze, Ridhiwani Kikwete ambaye ni mtoto wa Rais mstaafu wa awamu ya nne, Jakaya Kikwete amesema taarifa hizo zilitingisha familia yake, lakini baba yake Jakaya Kikwete alimtia moyo.

Ameyazungumza hayo katika mahojiano maalumu na Mwananchi Digital yaliyofanyika mwishoni mwa wiki iliyopita.

Tofauti na watuhumiwa wengine waliohojiwa kuhusu matumizi na biashara ya dawa za kulevya, Ridhiwani hakutangazwa hadharani badala yake aliitwa kimyakimya na kuhojiwa na baadaye kuruhusiwa aendelee na shughuli zake baada ya kuonekana hana hatia.

Hata hivyo aliongeza kuwa baba yake Mhe, Kikwete hakushtushwa na badala yake alimpa nguvu ya kwenda kueleza ukweli .”Pengine aliamua kuficha hofu yake ili kunitia nguvu,” amesema Ridhiwani.

Post a Comment

2 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad