Shilole Afunguka Kuhusu Ujauzito Wake...!!!


Msanii filamu na muziki wa bongo fleva, Shilole amefunguka na kuweka wazi kuwa yeye hana ujauzito wowote bali ameridhika na maisha jambo ambalo limefanya aongezeke mwili na kunenepa licha ya watu kuwa na hisia kuwa huenda ana ujauzito.

Shilole amesema hayo alipokuwa akihojiwa kwenye kipindi cha 5SELEKT kinachorushwa kila siku ya Jumatatu mpaka Ijumaa kuanzia saa kumi na moja jioni mpaka saa kumi na mbili kamili.

"Mimi saizi sina ujauzito wowote sema nimenenepa tu maana nimeridhika na maisha haya haya, ukimya wangu ni kwa sababu nilikuwa nazipa ngoma nafasi saizi nimeamua kuja rasmi na wimbo wangu huu 'sitoi kiki' kwani nimegundua Watanzania wanataka burudani, saizi pesa hakuna hivyo nimeona bora nije kuwaliwaza na muziki mzuri huu" alisema Shilole 

Mbali na hilo Shilole amesema video ya wimbo huo ataifanya na waongozaji kutoka hapa hapa Tanzania. 

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad