Warioba Apigilia Msumari Baa la Njaa Nchini...


Waziri Mkuu mstaafu, Jaji Sinde Warioba amesema haina haja ya kubishana kama kuna njaa au upungufu wa chakula kwani dalili zinaonyesha tatizo hilo litatupata na haitakuwa mara ya kwanza kwani limeshawahi kutokea.

Amesema kuwa wakati wa nyuma tatizo kama hilo lilipotokea watu walishirikiana kusaidia kuwapa wakulima maarifa na taarifa za hali ya hewa ili waweze kukabiliana na tatizo.

Ametolea mfano njaa inavyoathiri nchi za Somalia, Kenya na Nigeria kwa sasa ambapo watu na mifugo wamefariki na kusema mabishano hayasaidii.

Ameyasema hayo yote katika Kongamano la wanawake katika Uongozi linaloendelea katika ukumbi wa Makumbusho ya Taifa Jijini Dar es Salaam.
Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad