Baada ya CCM Kumpiga Stop Kusema Sema ..Nape Nnauye Ameibuka na Kuirushia Dongo Hili Serikali ya Magufuli..!!!


Mbunge wa jimbo la Mtama mkoani Lindi kupitia tiketi ya CCM, Mhe. Nape Moses Nnauye ametoa duku duku lake la moyoni kwa kusema kila anapokumbuka shida wanazozipata wananchi humfanya aonekane mkorofi kwa kuwa anasema ukweli.

Nape amebainisha hayo, kupitia ukurasa wake wa kijamii wa twitter huku akiwa ameambatanisha na picha ambayo inaonesha wananchi jinsi wanavyopata tabu kuvuka upande mmoja wa mto kwenda upande wa pili kwa kupita ndani ya maji hayo.

“Niliyashuhudia maisha haya mikoani kwa miezi 38, nadhani ndiyo nikiyakumbuka naonekana mkorofi !! iko haja kama Taifa kuangalia vipaumbele vyetu”. Ameandika Nape

Post a Comment

2 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.
  1. Good job bro keepitup

    ReplyDelete
  2. Leo baada ya kutumbuliwa ndio useme,Hasira tu.
    Mbunge wa ukweli hukemea mabaya wakati wote,muoneneni Bashe anavyotetea nchi.

    ReplyDelete

Top Post Ad

Below Post Ad