JPM Kunguruma Kilimanjaro Sherehe za Mei Mosi..!!


Rais John Magufuli amethibitisha  kuwa atakuwa mgeni rasmi katika sherehe za maadhimisho ya  siku ya Wafanyakazi (Mei Mosi) ambazo kitaifa zitafanyika mjini Moshi mkoani Kilimanjaro.

Akizungumza kwa niaba yake, Mkuu wa mkoa wa Kilimanjaro Said Meck Sadiki amesema kuwa Rais atakuwa mgeni rasmi katika sherehe hiyo,hivyo wananchi na wafanyakazi wajitokeze kushiriki na kusikiliza hotuba yake.

Sadiki amesema kuwa siku hiyo kutakuwa na huduma za  upimaji wa afya zilizoandaliwa na taasisi za afya hivyo aliwataka wakazi wa mkoa huu na watakaofika kutumia fursa hiyo kupima afya zao.


Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad