JULIAS Mtatiro: Baada ya Kujua Njama Zote Hizi Chama Chetu Kinajizatiti Kuchukua Hatua Hizi..!!!


OCD na OCCID wa Magomeni, wameelekezwa na mamlaka za juu (zisizotajwa) ati wawaite viongozi wa CUF (waliovamiwa jana na kundi la Mungiki la Lipumba), pamoja na Wavamizi (Lipumba na wenzake) ati OCD na OCCID wawapatanishe viongozi wa makundi hayo.

Baada ya maelekezo hayo, OCCID amewasiliana na viongozi waliovamiwa jana na MUNGIKI kuwaomba eti wakutanishwe na wavamiaji ili waombane radhi!

Yaani, wale wavamizi waliokuwa na bastola, mapanga, nondo na waya za umeme waliovamia mkutano wa jana na kuwapiga viongozi wa CUF na Waandishi wa Habari, eti majambazi hayo yapatanishwe na upande uliovamiwa (chama). Na wapatanishi ni POLISI.

This is so low and very stupid. Watu wamevamia mkutano halali kabisa wa chama, baada ya kuumiza watu na kuwatisha, wakakimbilia kwenye magari na kutokomea, eti watu hao sasa ni lulu na polisi inawalinda kweli kweli, hawagusiki!

Sasa mimi nawaambia POLISI, hebu wawasake wale Majambazi walioua POLISI wetu wasio na hatia kule Kibiti, wakishawapata majambazi hao, wapatane nao. I mean kwamba, POLISI wakapatane kwanza na wale majambazi waliotuulia vijana nane, ndipo waje kupatanisha haya majambazi ya jana VS Viongozi waliovamiwa/Waandishi wa Habari!

POLISI wameelekezwa wasimpeleke mahakamani Jambazi huyo alokamatwa na wameelekezwa wapotezee ile BASTOLA iliyooneshwa na yule Usalama wa Taifa aliyetumwa kuungana na MUNGIKI kufanya shambulio la jana.

Baada ya kujua njama zote hizi chama chetu kinajizatiti kuchukua hatua. Tunataka kuona Majambazi haya wanafikishwa mahakamani haraka na yaeleze ile Bastola ilikuwa ya nani? Hatuwezi kuwa na mazungumzo na watu wanaovaa kininja, wakipiga na kuumiza raia wasio na hatia.

Kama POLISI hawachukui hatua wanachofanya ni kuacha mambo haya yaendelee ili watu waanze kuuana, vifo vikishatokea eti ndiyo watasema kuna JINAI zimetokea. Sisi tunatimiza wajibu wetu. Shameful indeed!

JSM.

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad