MANENO Aliyoandika Mbunge Halima Mdee Kuhusu Tamko la Askofu Gwajima

Baada ya Askofu Mkuu wa Kanisa la Ufufuo na Uzima, Dr. Josephat Gwajima leo April 9, 2017 kumtaka Halima Mdee Mbunge wa CHADEMA kumuomba radhi Spika wa Bunge Job Ndugai kwa maelezo kuwa alimtukana, jioni hii kupitia Twitter ya Mbunge huyo ameandika kuhusu kinachoendelea kati yake na Spika Ndugai.

Mdee ameandika :
’Namuheshimu sana Mch. Gwajima,sitajibizana nae kwenye mitandao. Niweke rekodi sawa sijamtukana na wala sitarajii kumkosea heshima Spika.
 Hayo ya J2 namwachia yeye! Yangu na yaliyojiri Bungeni.. Najua jinsi ya kuyahandle. Yawezekana yalishamalizwa kabla ya Ibada yake LEO.

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad