MHE Mwigulu Hata Hili Nalo Utanyamaza..!!?


Wewe ndio kiongozi unayesimamia usalama wa RAIA na Mali zao ndani ya mipaka ya nchi. Sina mashaka na uwezo wako kiutendaji ila mashaka yangu ni jinsi ulivyo geuka bubu tokea upewe wizara hii na hasa unapo paswa kutolea kauli matukio yenye harufu za uhusika wa serikali.

Nikuulize tuu, jee na hili la uvamizi mkutano wa ndani wa CUF na watu kwenye silaha mbalimbali ikiwemo bastola nalo utanyamaza?

Anatajwa Lipumba kuhusika jee utahakikisha polisi wako wanamuondolea "kinga" ya kutokamatwa?

Tunajua pengine kuna uthibiti umefanywa dhidi yako ndio maana hufurukuti, lakini wewe bado kijana na una future katika siasa, mbona unakubali kuififisha? Hujui kimya chako (au woga) unakujengea picha kuwa wewe ni dhaifu na legelege asiye weza madaraka?

Ni katika kipindi chako tuu ndio tumeona silaha zinatolewa kweupe mchana na hakuna anaye chukuliwa hatua huku mamlaka zikihusishwa.

Fanya jambo Mwigulu na heshima yako itasimama juu bila kujali kwa sasa mteuzi atakufanyaje.

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad