Nani Anamkumbuka Msanii Ali Kiba?, Kwa Sasa Yupo Wapi?

Habari wakuu,

Ni kitambo sana msanii Ali Kiba hajasikika vinywani mwa watu, hajaonekana kwenye matukio yoyote na wala haandikwi kabisa na vyombo vya habari vya Tanzania, Afrika na hata dunia nzima.

Hata Jamii Forums nimejaribu kuangalia Jukwaa la ''Celebrities'' page ya KWANZA mpaka ya TANO hakuna mada inayomhusu moja kwa moja. Iliyopo kati ya Page hizo ni Kwanini Ali Kiba hataki bifu lake na Diamond liishe?.

Nilisikia ana show ulaya lakini sioni video wala picha mnato. Je, ni kwamba Show zimebuma mpaka anaogopa kuwaonesha mashabiki zake nini kinaendelea?

Mara ya mwisho katoa wimbo wa AJE na kaufanyia remix zaidi ya mbili, je ni kwamba kaishiwa utunzi?

#BringBackKingKiba

By Chachu Ombara

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad