Noma Sana..Husein Bashe Ashindwa Kuvuimilia..Afunguka Haya Mazito Kuhusu Sakata la Roma..!!!


Jana usiku taarifa za kukamatwa kwa msanii wa hip hop Roma Mkatolikia zilianza kuenea katika mitandao ya kijamii kwa kuripotiwa kuwa Roma Mkatoliki na Moni wakiwa studio za Tongwe Records walikuja kukamatwa na watu wasiojulikana na kuwapeleka kusikojulikana.

Watu mbalimbali ikiwemo wasanii mbalimbali wamekuwa wakionesha hisia zao juu ya tukio hilo kwa kutumia kurasa zao za mitandao ya kijamii kuoneshwa kuguswa na tukio hilo, mbunge wa Nzega Hussein Bashe ni miongoni mwa watu waliyotumia kuraza zao za instagram kuandika anachowaza kuhusu Roma.

"Who is behind all this? Ni genge ambalo limejipa mamlaka ya kupandikiza woga na chuki miongoni mwa jamii na kuharibu Taswira ya CCM. Tunawajibu wa kukataa woga ,Tunawajibu wa kutoruhusu Misuse ya vyombo vya Ulinzi na usalama, Tunawajibu wa kulinda Taifa letu

“Tunawajibu wa kupigania Values zilizopiganiwa na waasisi wa Taifa letu kama Mzee Karume na Mwl Nyerere, Tunawajibu wa kukataa ukandamizaji tukikaa kimya kwa kufikiri kuwa hayanihusu mimi yanamhusu yule yatakapokufika wewe hatakuepo mtu wa kukutetea na halitakuepo Taifa la Tanzania

“Sote tusimame tuseme hapana kwa mfumo huu unaoanza kuota mizizi kama mtu Ana makosa ufuatwe utaratibu wa kisheria kumkamata na sio utekaji tunakabiliwa na vita kubwa ya kupambana na Umasikini na kujenga Taifa huru la kiuchumi . 

"Umasikini ni hatari kwa usalama wa taifa sio nyimbo
#FreeRoma"
Tags

Post a Comment

2 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.
  1. Ubeberu ni unyama.kuna vibarska , wanafiki, badsla ya kukemea wengine wanstunga nyimbo kuzunguka wspate pesa zaidi. Ni lini watakuwa wazalendo na kuacha uswahili. Mtu katekwa. Mssnii mwenzao. Binadamu unatunga wimbo mavi .akili msli.

    ReplyDelete
  2. MH.Husein Bashe NA WEWE DAWA YAKO IKO JIKONI KM YA NAPE..NI UCHOCHEZI HUO UNAOLETA HUMU JAMVINI..HOW SURE YOU ARE AS GOV. DID THAT?Think before u talk mwanasiasa uchwala wee..nasema dawa yako iko jikoni lazima utainywa tu ili upone kabisa ..masifa yatakuponza hayo..nilimtabilia nape yakawa na wewe nshakutabilia...

    ReplyDelete

Top Post Ad

Below Post Ad