Sehemu za Siri za Maiti ya Mama Mjamzito na Matumizi Yake Katika Ulozi..!!


Nikiwa katika kijiji cha kabila wilayani Magu enzi za ujana wangu mwishoni mwa miaka ya tisini, kwa mara ya kwanza nilikwenda nilikwenda kwa mganga nikiwa nimefuatana na shangazi yangu baada ya aliyekuwa mtoto wa shangazi yaani Binamu kufa katika mazingira ya kutatanisha.Baada ya kupigiwa ramli na mganga kupitia kifaa maalum yaani cha kupigia ramli (Shelo) na kifaranga tukagundua ndugu yetu alikufa kwa kuchochewa nafsi ili akajitupe bwawani tuamini amekufa na wachawi wamchukue kirahisi (kusonelwa).

Baada ya ramli mganga akatushauri tufanye zindiko la kumfnya ndugu yetu asibaki msukule ila tummalizie afe kabisa na asiendelee kuteseka huko alikofichwa ktk kijiji jirani cha jinjimili. mganga alitusihi tutafute kuku wa rangi nyekundu yaani (Shingamageji),mafuta ya simba,mchanga wa kaburi la mtu aliyekufa kwa kukujinyonga, mtama na sehemu za siri za mwanamke aliyekufa na ujauzito wake.

Zindiko lilianza mnamo saa moja na nusu usiku ili tuwahi kabla mida ya wachawi hawajafka kisha tuweke kingo za kuwazuia wasisogee eneo la zindiko ambalo lilipaswa kuisha kabla jogoo wa kwanza hajawika ambaye ndo hutumika kama alarm ya wachawi kuondoka na ikitokea jogoo wa pili amewika huyo mchawi amechelewa na lazima atashindwa kurudi na asubuhi ataumbuka.

Tulipofika eneo la zindiko mganga alisimama juu ya kaburi sisi wengine wawili tukakaa upande wa magharibi kwa direction ya kichwa cha kaburi kilipoelekea. Tulimchinja jogoo mwekundu kisha damu yake ikazungushiwa eneo la zindiko kisha tukajichanja na kujiwekea mafuta ya simba kama zindiko ili wachawi wasitusogee japo walikuwa wanatuona sana.mganga alirusha mtama angani kisha kisha ule mchanga wa kaburi la mtu aliyejinyonga akaumwaga juu ya kaburi la ndugu yetu ambapo ndo lilikuwa hasa eneo la zindiko.

Baada ya kuumwaga ule mchanga kwa juu yake tukaziweka sehem za siri za mwanamke aliyekufa akiwa na mimba kisha tukaanza kuziunguza wakati zinaungua mganga aliongea maneno mengi huku akitaja jina la marehemu binamu yangu.cha ajabu zile sehemu za siri hazikuisha na ziliteketea kwa zaidi ya masaa sita.wakati zinateketea mganga alitoa ngozi ya fisi na ndani ya ngozi kilifungwa kifundo cha nyama kubwa kavu ya moyo wa binadamu ambayo tuliipaka dawa kisha mganga akaiweka juu ya zile sehem za siri zilizokuwa zinateketea akatuasa tuwe makini tusishtuke kwani muda si mrefu ile nyama ya moyo ingemezwa na uke unaoteketea halafu baada ya saa moja uke uendelee tena kuungua kisha kuna mlio mkubwa wa kupasuka utoke na hapo ndipo binamu angekufa kabisaa asiendelee kuwa msukule.

Kweli baada ya hilo tukio kutokea nikishuhudia ikiwa ni majira ya saa saba usiku tulikaa kmya mganga akatusihi tuinamishe vichwa na alipotuambia tuinue tukawaona mtoto mmoja na mama mmoja wako uchi wamesimama na kisha walichukua ule uke tulioumaliza kuutumia kwenye zindiko kisha wakaondoka.baada ya tukio hilo mganga akatuambia ile ni misukule ilitumwa na waliomroga ndugu yetu kuja kuchukua hicho kiungo kama ishara ya wao kukubali kuwa binamu yetu amekufa na pia kuashiria amani na mganga maana waganga na wachawi ni mahasimu ambao ni hupatana pia muda mwingine.

Huo ndio ukawa mwanzo wangu wa kujua mengi sana niyajuayo sasa kuhusu uchawi katika ardhi ya Usukuma
Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad