Ukweli Mchungu..Roma na Wenzako, Msithubutu Kuwasariti Wapiga Yowe Wenu..!!!!


Kitendo chenu cha kuficha ukweli wa mambo ulivyo, eti kwa sababu ya mapatano na watekaji; 

Mosi.
Huku kutakuwa ni kuwasariti wale walioshinikiza kuachiwa kwenu, na ni dhambi mbaya sana!

Pili.
Kitendo cha kuficha ukweli wa mambo ulivyo;
Huko kutakuwa ni kuridhia ndugu zenu na jamaa zenu waendelee kutendewa kama ninyi au zaidi yenu, yaani kupotezwa kabisa kama Ben.

Tatu.
Kitendo cha kuficha ukweli wa yale yaliyowakuta;
Huko kutakuwa ni kuiridhia dhambi ya watekaji.

Nne. kitendo cha kudanganya ili kuficha dhamira ya watekaji;
Huko kutakuwa ni kumkosea Mungu aliyewatoa katika makucha ya simba wenye uchu wa nyama zenu.

Mwisho.

Roma mkatoriki, mnamkumbuka Dr. Ulimboka?

Nani ajuae huenda angeweka ukweli wa mambo yaliyomkuta wazi leo msingekuwa wahanga wa haya!

Narudia. 
Semeni ukweli ili kuwatia moyo watetezi wenu kusudi waendelee kuwapambania wengine.
Semeni ukweli maana wasema kweli ni wapenzi wa Mungu.
Tags

Post a Comment

1 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.
  1. hii ni kama kamchezo Fulani za kiki mbona hata wasiwasi hawana ni kweli walitekwa na kwa sababu gani hiyo nchi ni ya VITUKO watu wako ki mzaha mzaha mnaweza mkasababisha mauwaji ya kweli watu wakadhani ni yale yale semeni watu wachukuliwe HATUWA ZA SHERIA

    ReplyDelete

Top Post Ad

Below Post Ad