WATANZANIA Tuwe na Huruma, Tuwasamehe Bongo Movie

Habari ya wakati huu wakuu.

Sisi watanzania tunafahamika kwa ukarimu na roho nzuri, upendo na kusaidiana, tabia ambayo mwalimu alitufundisha.

Lakini pia sisi ni watu wabaya sana kama mtu atatuudhi, kwa jinsi watanzania mlivyowawakia bongo muvie ni dhahiri kua hao watu wametukwaza sana.

Bongo movie wametuudhi na kutughadhabisha sana, katika mitandao yote inayofahamika hapa nchini na blogs naona ni kuwashambulia wasanii wa bongo movie.

Mimi niwaombe ndugu zangu, hawa ni ndugu na jamaa zetu, ni wanetu na wazazi wetu, kama ni watu wenye akili saaa watajirekebisha kwa jinsi walivyosakamwa iwa kazi yao mbovu na kujiingiza katika vita isiyowahusu ya kurubuniwa na DAB mtu ambae amekosa ile wataalam wanaita "moral authority" ya kukemea au kuelekeza lolote liwe baya au zuri kutokan na kukosa kuaminika.

Niombe, hawa watu kama wana akili watajirudi, najua wametambua makosa yao, naomba tuwasamehe tuwape nafasi nyingine vinginevyo tutawaua kwa msongo wa mawazo na msukumo mkubwa wa damu.

Imetosha, tumewasema vya kutosha, kila mahali ukifungua watu wanaponda tu hawa bongo movie, tuwahurumie ndugu zangu, wao pia ni watu wanafanya makosa kama sisi sote tunavyofanya makosa.

Ni hayo tu ndugu zangu.

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad