Ajali ya Karatu sio ishu ya kisiasa- RC Mrisho Gambo


Mkuu wa Mkoa wa Arusha, amesema kuna watu wanatumia mitandao ya kijamii wakiwa na lengo kuu lakutaka kuyumbisha lengo la serikali la kuwahudumia majeruhi wa ajali ya gari ya shule ya Lucky Vicent ambao leo wamesafirishwa kwenda Marekani kwa matibabu.


Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Mrisho Gambo


Mrisho Gambo akiongea uwanja wa ndege wa KIA amewataka watu wa Arusha na Watanzania kwa ujumla kuendelea kuungana na kuwa wamoja katika lengo hilo ili kuhakikisha watoto hao wanapata huduma nzuri huko waendako na kurudi nchini salama ili baadaye waje kutumikia taifa lao la Tanzania. 


"Tunauhakika huko wanakokwenda watatibiwa vizuri na kurudi salama Tanzania ili kulitumia nchi yao, hili tukio siyo tukio la kisiasa tusikubali mtu yoyote kwa sababu yoyote atutoe kwenye lengo la msingi la kutoa huduma kwa watu wetu, wakati sisi tunahangaika kwenda kuzika watu, tunahangaika na kuhakikisha watu wanasafiri kwenda kutibiwa kuna watu wengine wanatumia mitandao ya jamii kutaka kupoteza focus ya serikali na watu wengine kuhakikisha kwamba wahusika wetu wanapata matibabu bora na wanabaki salama kwa hiyo nitumie nafasi hiii kuwaomba watu wa Arusha na watanzania wote tuendelee kuungana na kuwa wamoja kuhakikisha kwamba tunaikamilisha kazi hii ya Mungu" alisema Gambo  

Post a Comment

2 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.
  1. Ni lini hizi ajari za kijingakijinga zitakoma!!??

    ReplyDelete
  2. siasa ya lema ingekuwa kingiza cdm hala pia hajitambui

    ReplyDelete

Top Post Ad

Below Post Ad