BAADA ya Askari Nane Kuuawa Pwani..Serikali Yaanzisha Mkoa Mpya wa Kipolisi Rufiji..!!!


Serikali imetangaza kuanzisha mkoa mpya wa kipolisi katika wilaya za Mkuranga, Kibiti,  Rufiji na Mafia ili kuimarisha usalama katika maeneo hayo.

Waziri wa Mambo ya Ndani, Mwigulu Nchemba amelieleza Bunge leo (Jumanne) katika hotuba yake ya Makadirio ya Mapato na Matumizi kwa mwaka 2017/18.

Nchemba amesema mkoa huo utaitwa Mkoa wa Kipolisi Rufiji.

Kibiti kumekuwa na matukio mbambali ya mauaji ambayo yamegharimu maisha ya baadhi ya wananchi.

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad