BREAKING: Hans Poppe wa Simba Sc abwaga manyanga


Aliyekuwa Mwenyekiti wa Kamati ya Usajili Simba, Zacharia Hans Poppe ameachia ngazi.


Habari za uhakika zimeeleza kuwa Hans Poppe ameandika barua ya kuachia ngazi kwa madai kuwa anaona mambo yanaendeshwa ndivyo sivyo.


Chanzo chetu cha kuaminika kinaeleza kuwa "Hans Poppe ameachia ngazi kwa kuwa hakufurahishwa na mlolongo ulivyokuwa hadi Simba kuingia mkataba wa SportPesa,” kilieleza chanzo.


"Hans Poppe ameandika barua kujiuzulu kwenye kamati ya utendaji, maana yake anaondoka moja kwa moja katika nafasi ya mwenyekiti wa kamati ya usajili.


"Kilichomchukiza, anasema kuna kundi lililoongozwa na Rais Evans Aveva na makamu Geofrey Nyange Kaburu, lilifanya mambo kimya kimya na Hans Poppe amesema hata Mo Dewji aliyeisaidia Simba mishahara naye hakushirikishwa hata kiungwana tu, hivyo amepinga hilo."
Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad