Diamond: Sitaki Tiffah Awe Msanii, Naogopa Ataliwa Sana na Wanaume...!!!


Diamond Platnumz amefunguka kwa kudai kuwa hataki mtoto wake wa kike Tiffah awe msanii kwa madai akiwa msanii atatembea kimapenzi na wanaume wengi.

Muimbaji huyo amedai mtoto wake huyo akiwa msanii, wanaume wengi watamiminika kumtaka kimapenzi.

“Mtoto wangu wa kiume ningependa awe msanii lakini mtoto wangu wa kike sitaki awe msanii, watamla sana,” alisema Diamond weekend iliyopita  akiwa katika kipindi KTN nchini Kenya. 

“Mtoto akiwa msanii watu wanaomjua wanakuwa wengi, watu wanaokujua wakiwa wengi na kutongozwa kunakuwa kwingi, sasa watanipa presha,”

Aliongeza, “Ukiwa mwanaume lijali na ukiwa kwenye nafasi kama yangu lazima wataliwa. Nilikuwa kwenye kutafuta tafuta, mpaka nilivyompata Zari na kweli nimetulia,”

Muimbaji huyo Jumanne hii anatarajia kuhudhuria mazishi ya aliyekuwa mume wa Zazi, Ivan aliyefariki wiki iliyopita nchini Afrika Kusini kwa ugonjwa wa moyo.

Post a Comment

1 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.
  1. Haya bwana chibu MKUKI KWA NGURUWE wewe wakati unawapiga watoto wa watu uliona watamue hapo hata kama siyo msanii atapigwa mbaya

    ReplyDelete

Top Post Ad

Below Post Ad