KALA Jeremiah Atangaza Nia ya Kugombea Urais..!!!


Msanii wa muziki wa hip hop, Kala Jeremiah amefunguka kwa kusema kuwa hawezi kugombea ubunge kwani tayari ameshafanya kazi hiyo kwa miaka mingi na sasa anasubiri muda ufike aweze kugombea nafasi ya Urais.

Akiongea na umati wa watu uliojitokeza katika show ya ‘Wapo Tour’ya rapa Nay wa Mitego iliyofanyika Dar Live weekend hii, Kala atiwata mashabiki wake wajiamini katika mambo yao kama yeye anavyoamini siku moja anawekuwa Rais.

“Urais ndiyo ishu kwa sasa, kusema ukweli tayari nimeshakuwa mbunge kwa miaka mingi hata mashabiki wangu wanajua. Lakini kusema tena niende kugombea ubunge hapana siwezikufanya hivyo kwa hadhi yangu. Nafasi ya Urais ndiyo nayoitaka lakini siwezi kusema ni lini ila jua ipo siku mimi nitagombea nafasi hiyo,” Kala aliiambia alisema muda mchache baada ya kushuka kwenye steji.

Rapa huyo amedai hakuna kitu kinachoshindikana kwenye dunia kama mtu akiamua kufanya jambo lake.

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad