Godbless Lema Afunguka 'Yeriko Nyerere Amekamatwa au Ametekwa?'

Mbunge wa Arusha Mjini (Chadema) Godbless Lema ameuliza swali je, Yeriko Nyerere amekamatwa au ametekwa?

Lema ameuliza swali hilo katika ukurasa  wake wa Twitter leo na kuongeza: “Msiogope. Lakini kwa kadiri ya walivyowatesa ndivyo walivyoongezeka na kuzidi kuenea. "

Yeriko anayefahamika kuwa ni kada wa Chadema, amekamatwa leo saa tisa alfajiri na watu wanaodhaniwa kuwa ni polisi akiwa nyumbani kwake, Kigamboni, Mbutu.

Meya wa Ubungo, Boniphace Jacob amethibitisha kukamatwa kwa Yeriko.
Yerico amekamatwa au ametekwa ? MSIOGOPE. Kwani imeandikwa "Lakini kwa kadiri ya walivyowatesa ndivyo walivyoongezeka na kuzidi kuenea "
— Godbless E.J. Lema (@godbless_lema) May 31, 2017

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad