LITA 50,000 za Mkojo Zatumika Kutengeneza Pombe..!!!


Kiwanda kimoja cha pombe nchini Denmak kimetengeneza bia mpya kwa kuchanganya ngano na lita 50,000 za mkojo.

Hata hivyo bia hiyo haitakuwa na mkojo wa binadamu.

Mkojo huo ulikusanywa  kwa watu waliokuwa kwenye  hafla moja kubwa zaidi ya muziki barani ulaya miaka miwili iliyopita

"Wakati habari ziliposambaa kuwa tulikuwa tumeanza kutengeneza pombe, watu walidhani kuwa tulikuwa tukiweka mkojo huo moja kwa moja  kwenye pombe," alisema Mkurugenzi wa kampuni ya Norrebro Bryghus inayotengeneza pombe hizo.

“Kama ingekuwa na ladha ya mkojo ningeachana nayo, lakini hata huwezi ukahisi," alisema mtu moja ambaye alihudhuria warsha hiyo ya muziki mwaka 2015.

Lita hizo 50,000 zilizokusanywa kutoka kwa warsha hiyo ya muziki zilitosha kuunda chupa 60,000 za bia.

Mashine iliyotengenezwa na kundi la wanasayansi katika chuo kimoja nchini Ubelgiji, inabadili mkojo wa binadamu na kuwa maji ya kunywa pamoja   kwa kutumia nguvu za miale ya jua.

 Chanzo BBC.
Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad