MMILIKI wa Lucky Vicent na Makamu Mkuu wa Shule Ambayo Wanafunzi Wake 33 Walikufa Ajalini Arusha Waachiwa kwa Dhamana..!!!


Mmiliki wa shule ya msingi Lucky Vincent,Innocent Mosha amefikishwa mahakamani jana  mjini hapa kujibu makosa manne  yaliyosababishwa na  ajali ya basi lake lililouwa watu 35 wakiwamo wanafunzi 32.

Pia makamu Mkuu wa shule hiyo,Logino Vicenti amepandishwa kizimbani kujibu shitaka moja la kuongeza abiria 13 kwenye gari lililopata ajali.

Mwendesha mashitaka Rose Sulle  ameiambia mahakama mbele ya hakimu mkazi Desderi Kamugisha kuwa  upelelezi wa kesi hiyo haujakamilika.

Watuhumiwa  wamepata dhamana kila mmoja yenye thamani ya Sh 15 milioni. Kesi itatajwa tena Juni 8 mwaka huu.

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad