PICHAZZ...Zari Ashindwa Kuvumilia ..Amfuata Mume Wake wa Zamani Hospitali...!!!!


Mama watoto wa Diamond, Zari the Bosslady ameonekana katika picha akimjulia hali ex wake Ivan Ssemwanga ambaye anadaiwa kulazwa katika hospitali moja nchini Afrika Kusini baada ya kupata matatizo ya moyo.

Ivan ambaye alipata watoto watatu na Zari, anadaiwa kukimbizwa hospitali wiki hii baada ya kupoteza fahamu.

Jumatatu hii Zari alipost picha ya mshumaha na kuwaomba mashabiki wake kumuombea mzazi mwenzake huyo.

Hapo jana Zari kupitia ukurasa wake wa SnapChat aliandika “Siku mbili kwangu zimekuwa ngumu, nawaomba tumuombee Ivan”.

Mitandao ya Uganda inadai kuwa Ivan anasumbuliwa na maradhi ya Shambulio la Moyo (Coronary Artery Disease).

Post a Comment

1 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.
  1. Pole sana na hongera mke wa Diamond kwa kumjulia hali huuo mzazi mwenzako, huo ndiyo ubinadamu hata kama alikukosea vipi.

    ReplyDelete

Top Post Ad

Below Post Ad