RASMI..Kitwanga Atakiwa Ahame CCM..Ni Baada ya Kusema Kuwa Ataenda Kuharibu Mitambo ya Maji ya Ziwa Victoria Bungeni..!!


SIKU chache baada ya Charles Kitwanga kutishia kuzima mtambo wa kusukuma maji kutoka Ziwa Victoria kwenda mikoa ya Shiyanga na Tabora, serikali imemjibu waziri huyo wa zamani wa Mambo ya Ndani ya Nchi kwa kumtaka ahame kwenye chama tawala, Chama Cha Mapinduzi (CCM) kama anaona hatendewi haki.

Akichangia mjadala wa makadirio ya mapato na matumizi ya Wizara ya Maji na Umwagiliaji bungeni mjini hapa Jumatano, Kitwanga alitishia kuhamasisha zaidi ya wananchi 10,000 kwenda kuzima mtambo wa maji ulioko kwenye chanzo cha maji cha Iherere jimboni kwake Misungwi, mkoani Mwanza, ikiwa hawatapatiwa maji yatokanayo na mradi huo.

Hata hivyo, Waziri wa Maji na Umwagiliaji, Mhandisi Gerson Lwenge, akihitimisha mjadala wa makadirio hayo juzi. alimjibu mbunge huyo kwa kumtaka aihame CCM kama anaona hakitendi haki dhidi yake.

"Mheshimiwa Naibu Spika, naomba nizungumzie suala la mchango wa Mheshimiwa Kitwanga. Amechangia hapa kwa hisia kubwa kuonyesha kuwa serikali ya CCM haijafanya chochote kwenye Wilaya ya Misungwi," alisema.

"Sasa nataka nimuulize Kitwanga kama yupo hapa kwamba hayo ni maneno yake au ya wananchi? Kama ni ya wananchi nitawaambia ni nini kimefanyika Misungwi kwani hata juzi tumetia saini mikataba ya maji na Mwenyekiti wa Halmashauri alikuwapo, ya kupeleka maji Misungwi kutoka Ziwa Victoria kwa fedha nyingi zaidi ya Sh. bilioni 38.

"Sasa anaposema anakwenda kuhamasisha wananchi wakabomoe mtambo wa Iherere, maana yake analeta uasi au hathamini kazi iliyofanywa na chama chake, sasa ajitoe kwenye chama kwa sababu serikali imepeleka fedha na maendeleo yaliyofanyika ni lazima tuwahamasishe wananchi kutunza miundombinu iliyopo badala ya kwenda kuibomoa.

"Hata kwenye umeme huwa tunaona wanaweka kwenye kijiji kimoja na kuruka hadi kijiji cha nne, lakini hatujawahi kuona wanang'oa nguzo. Sasa nataka nimwambie serikali inaendelea kuboresha maji katika maeneo mbalimbali ikiwamo Misungwi na Usagara."

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad