SAKATA la Mauaji ya Kibiti ..Polisi Waja na Mbinu ya Kuwajaza Watu Mamilioni Ili Kuwafichua Wahusika..!!!


JESHI la Polisi mkoa wa Pwani limetangaza zawadi ya Sh. milioni tano kwa mwananchi ambaye atafanikisha kukamatwa kwa watuhumiwa 12 ambao limedai wanajihusisha na mtandao wa mauaji yanayoendelea katika Wilaya za Kibiti, Mkuranga na Rufiji.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Pwani, Kamishna Msaidizi Mwandamizi Onesmo Lyanga, aliwaambia waandishi wa habari jana kuwa Jeshi hilo linaendelea kuwasaka watuhumiwa hao.

Alisema Polisi imepata picha za baadhi ya watuhumiwa na fununu za mahali wanapopenda kutembelea mara kwa mara.

MAJINA YA WATUHUMIWA

Kamanda Lyanga aliwataja watuhumiwa hao pamoja na mwanzilishi wa mtandao huo wa mauaji kuwa ni Abdurshakur Ngande Makeo, Faraj Ismail Nangalava, Anaf Rashid Kapera, Said Ngunde na Omary Abdallah Matimbwa.

Wengine ni Shaban Kinyangulia, Haji Ulatule, Ally Ulatule, Hassan Uponda, Rashid Salim Mtulula, Sheikh Hassan Nasri Mzuzuri na Hassan Njame.

“Jeshi letu limewabaini watuhumiwa hao kwa kushirikiana na wasiri wetu huku tukiendelea na uchunguzi zaidi," alisema Kamishna Lyanga.

Alisema polisi imegundua kuwa watuhumiwa hao hupendelea kutembelea maeneo ya kisiwa cha Simbaulanga, kisiwa cha Saninga katka kijiji cha Nchinga na kijiji cha Mfesini kata ya Nyamisati pamoja na maeneo mbalimbali ya wilaya za Kibiti, Rufiji na Mkuranga.

Kamishna Lyanga aliwataka wananchi kuendelea kutoa ushirikiano wa kuwafichua watuhumiwa wote wa mtandao ambao unahatarisha hali ya usalama mkoani hapa.

Credit - Nipashe
Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad