WAZIRI Mwakyembe: Msanii Anayetaka Kuzungumzia Siasa, Akagombee Ubunge au Udiwani

Akijibu hoja ya Profesa Jay kuwa wasanii wakiimba nyimbo za siasa kuhihoji serikali wamekuwa wakinyanyaswa ila wakiimba nyimbo za kuisifia tu wanaachwa Mwakyembe amejibu kuwa wasanii hawatakiwi kuimba nyimbo za siasa na kama wanataka kuzungumzia siasa basi wagombee udiwani au ubunge.

Amesema hakuna mwanamuziki yoyote duniani aliyefanikiwa kwa kuikandia serikali, ametembelea nchi kama Nigeria na wasanii waliofanikiwa kama wakina P Square,Tiwa Savage, Davido ni wasanii wenye mafanikio lakini hawajapata mafanikio hayo kwa kuitukana serikali.

Muziki ni entaritainment industry na sio political Indusrty na hata Afrika Mashariki wasanii kama Chamilione na akina Diamond na Ali Kiba wana mafanikio lakini hawaimbi siasa.

Amemtolea mfano msanii mmoja Fella Ramson Kuti aliyeimba siasa na akaishia pabaya.


 SIKILIZA HAPA:

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad