Kifungu cha 9(3) cha Sheria ya Madini (2010) ni Msumari wa Moto Lakini Wala Hakikutajwa na Kamati ya Pili ya Mchanga wa Madini...!!!!


Labda tujiulize hivi kwanini kamati ya pili haikujiridhisha na kifungu cha 9(3) cha sheria ya madini ya mwaka 2010?

Kifungu tajwa kinamwondelea Mchimbaji wa madini aliyesajiliwa uhaja wa kusajili tena kampuni tanzu katika kufanya kazi za uchimbaji, usafirishaji wa madini.

Kwa lugha rafiki, baada ya African Barrick Gold Ltd kusajiliwa kuwa ni mmiliki wa North Mara Gold mine Ltd, Bulyanhulu Gold mine Ltd na Pangea Minerals Ltd ambapo migodi yote imesajiliwa hawakuwa na uhaja tena wa kusajili kampuni tanzu yake ya Acacia.

Sasa sijui walimeza maharagwe ya wapi hii kamati ya pili ya Makinikia kudai Acacia ilipaswa isajiliwe wakati sheria ya madini (2010), kifungu na. 9(3) kinawazuia wasisajili tena kampuni tanzu.

Chanzo JF

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad