Simba Sc Yasajili Wawili Kutoka Mwanza..Kaburu Adai Anamajina Mengine Sita Makubwa Yatasaini Simba Hivi Karibuni..!!


Klabu ya Simba SC imeanza kuimarisha kikosi chake kuelekea msimu ujao wa Kombe la Shirikisho la Afrika, baada ya jana kukamilisha usajili wa walinzi wawili kutoka jijini Mwanza.

Simba imevuta beki wa kushoto, Jamal Mwambeleko kutoka Mbao FC na beki wa kati Yussuf Mlipili kutoka Toto Africans ambao wote wametokea jijini Mwanza

Kwa mujibu wa Makamu wa Rais wa Simba SC, Geoffrey Nyange ‘Kaburu’ amesema kwamba, Mlipili amesaini miaka mitatu na Mwambeleko amesaini miaka miwili adai mchezaji Mlipili anatua kwa mara ya kwanza kabisa Simba SC, wakati Mwambeleko yeye ni kama anarudi nyumbani sababu amewahi kuchezea timu ya vijana ya Wekundu hao wa Msimbazi.

Mbali na hilo Kaburu baada ya kukamilisha usajili huo amesema mashabiki na wapenzi wa Simba wakae mkao wa kula kwa taarifa za kuvutia zaidi kuhusu usajili wa timu yao hiyo ambao unaendelea sasa.

“Kwa ujumla nina wachezaji sita ambao wamekwishakamilisha usajili wao hapa Simba, lakini nitakuwa nachomoa mmoja mmoja namtambulisha” Alijinasibu Kaburu 

Mlipili na Mwambeleko wote waliichezea Simba SC kwa mara ya kwanza kwenye mashindano ya SportsPesa Super Cup 2017 huku Simba ikitolewa kwa penalti 5-4 na Nakuru All Stars ya Kenya.

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad