Ukweli Mchungu...Pamoja na Kuijenga CHADEMA kwa Mikono Yake, Ndesamburo Hakupewa Heshima Kama Lowassa na Sumaye..!!!


Marehemu Mzee Ndesamburo kama almaarufu kama Ndesa Pesa, ni watu waliojiondoa CCM mara baada ya vyama vingi kuanza rasmi nchini Tanzania, huku akiwa muasisi na mwenyekii wa kwanza wa Chadema mkoa wa Kilimanjaro. Alikijenga chama huku Sumaye akiwa waziri mkuu alitamka kejeli akiwa katika ziara mkoani Kilimanjaro miaka ya mwanzoni 2000 kuwa ''ukitaka biashara yako ifanikiwe jiunge na CCM''.

Ndesamburo alitumia rasilimali zake na ushawishi kuijenga Chadema katika kipindi chote hicho bil kuchoka, Huku akiwa Mwenyekiti wa Mkoa alikuwa pia mjumbe wa Baraza kuu la chama Taifa hivyo kimadaraka ndani ya chama ni 'mzito' kuliko akina Lowassa na Sumaye ambao kimsingi walikuja kugombea uraisi na si kuijenga Chadema.

Haikuwahi kutokea katika uhai wake Mzee ndesamburo kukaa meza kuu lakini ghafla wajumbe wapya wawili wasio viongozi wa sekretariet wanaketi meza kuu huku Mzee Ndesamburo akiketi viti vya nyuma kabisa.

Upumzike kwa amani Mzee wangu Ndesamburo, Leo kila mtu anataka kupata sifa na umaarufu kupitia msiba wako wakati walikutenga kipindi cha uhai wako.

Chanzo JF

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad