VIDEO:Vanessa Mdee Aweka Wazi Kutosana na Juma Jux.....

Mwanamuziki Vanessa Mdee amezungumza hadharani kwa mara ya kwanza kuwa hayupo tena katika uhusiano wa kimapenzi na Juma Jux maarufu Jux.

Vanessa amesema kuwa, mambo mengi yalitokea na hivyo kupelekea wawili hao ambao walikuwa wakiwavutia wengi (best couple) kuvunja uhusiano wao wa kimapenzi.

Vee Moneya au Cash Madame ameyasema hayo alipokuwa akifanya mahojiano na kituo cha redio cha Soundcity kilichopo nchini Nigeria alipokwenda kwa ajili ya shughuli zake za muziki.

Kwa muda mrefu kupitia mitandao ya kijamii watu wamekuwa wakidai kuwa wawili hao waliotamba na wimbo wa JUU waliokuwa wakiimbiana hawapo tena pamoja, lakini wao wenyewe hawakuwahi kuzungumzi jambo hilo au kuonyesha ishara yoyote ambayo ingethibitisha kuwa wameachana.

Hapa chini ni sehemu ya mahojiano hayo, ambapo Vee Money alikiri kumwagana na Jux;


Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad