Zifahamu Aina za Vyakula Vinavyoongeza Uhodari kwa Wanaume..!!!


Vyakula jamii ya nafaka ni miongoni mwa vyakula ambavyo vimejaa nishati nyingi ikiwa ni pamoja na nyuzinyuzi na sukari. Hivyo unaweza kuweka kwenye orodha ya vyakula anavyopaswa kula mwanaume.

Nafaka husaidia kuzalisha homoni ya testosterone kwenye damu hivyo kumuwezesha mtu kuwa na nguvu na hivyo kuepuka tatizo la upungufu wa nguvu za kiume.

Ulaji wa vyakula vya nafaka visivyokobolewa ni muhimu zaidi kwani husaidia kutokupa mwili wa mafuta mengi kwani mafuta mengi ndani ya mwili huweza kuchangia kuharibu mishipa ya damu ikiwamo mishipa uume.

Moja ya viungo muhimu kwa wanaume ni pamoja na tangawizi ambayo husaidia kusisimua mfumo wa mzunguko wa damu mwilini ieleweke kwamba mzunguko wa damu unapokuwa vizuri ndani ya mwili husaidia hata damu kwenda vizuri sehemu za viungo vya uzazi pia (uume).

Aidha, ulaji wa karanga ni muhimu pia kwani ndani ya karanga kuna madini ya magnesium,zinc ambayo ni muhimu sana katika uzalishaji wa mbegu za kiume pamoja na kuamsha hisia za tendo la ndoa.

Pia matumizi ya tunda la komamanga huweza kumsaidia mwanaume kujenga afya ya kimahusiano kutokana na tunda hilo kusaidia kuamsha mishipa ya fahamu na hivyo kumuongezea mtu uwezo wa kushiriki tendo hilo.

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad