BLACk Chyna Kumpeleka Rob Kardashian Mahakamani..Kisa Picha za Utupu

Mwanamitindo na mfanyabiashara Angela Renee White a.k.a Blac Chyna, amemfungulia mashtaka mpenzi wake Rob Kardashian.
 

Blac Chyna ambaye amezaa mtoto mmoja na Rob, wiki hii amejikuta akipokea mvua ya matusi na udhalilishaji pamoja na picha zake za utupu alizokuwa akimtumia mpenzi wake kuwekwa hadharani katika mtandao wa Instagram na mwanaume, ambaye anamtuhumu mpenzi wake huyo kuwamsaliti kwa kuwa na wanaume wengine kuwa mtumiaji wa madawa ya kulevya.

Mwanasheria wa mrembo huyo, Lisa Bloom ametumia ukurasa wake wa twitter, kutweet kwa kumjulisha Rob kuwa anatakiwa kufika mahakamani jumatatu kujibu tuhuma zinazomkabili za kumdhalilisha mpenzi wake huyo wa zamani.

“I represent Blac Chyna. I just gave Rob Kardashian notice that we’ll be in court Monday seeking restraining orders against him. More to come,” ameandika mwanasheria wa Blac

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad