Jina la Malinzi lafutwa kugombea Urais TFF


Jumamosi ya July 8 2017 kamati ya uchaguzi ya shirikisho la soka Tanzania TFF ilikutana kwa mara ya kwanza baada ya kuvunjwa na kuundwa upya na kikao cha kamati ya utendaji ya TFF.


Kamati ya uchaguzi ya TFF leo imekaa na kikao chake kimemalizika jioni ya leo na kufanya usahili wa wagombea wa nafasi zote na kuchuja, list ya wagombea waliyochujwa nafasi ya Urais ni pamoja na Rais wa sasa wa TFF Jamal Malinzi ambaye amechujwa kwa kukosekana katika usahili.


Malinzi amekosekana katika usahili kutokana na kuwa rumande kwa kesi ya tuhuma ya makosa 28 kati ya hayo 25 yana muhusu yeye ikiwemo tuhuma ya utakatishaji fedha ambayo imesababisha kukosa dhamana kwa mujibu wa sheria.
Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad