Mwanamuziki Peter Msechu Alia na Clouds FM...Adai Ananenepa Kwa Vile Hapati Show.....

Msanii wa Bongo Flava, Peter Msechu amedai kuwa ananepa kwa sababu hafanyi show.


Muimbaji huyo ambaye ameachia ngoma mpya ‘Yakawa’, ameiambia XXL ya Clouds Fm licha ya kukosa show lakini bado anajitahidi kupunguza unene na kuna baadhi ya watu wamekuwa wakiomba ushauri kwake kujua namna ya kupungua.

“Nanenepa sometime sio kwamba sifanyi mazoezi, ni kwamba nakosa show, nikija jukwaani nikiruruka napungua,” amesema Msechu.

Pia ameongeza kuwa, “sasa hivi nimepungua kuna jamaa jana wamenicheki kwenye mtandao anaulizia namna ya kupungua. Sasa nina kg kama 120 nilikuwa na kg 160”.
Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad