Polisi Dar watia Mbaroni Madalali Bandia 12 Wanaojihusisha na Wizi wa Shehena za Bidhaa

Jeshi la Polisi Mkoa wa Kipolisi wa Temeke jijini dsm linawashikilia madalali bandia 12 wanaodaiwa kuendesha vitendo vya wizi wa shehena za bidhaa za mamilion ya fedha huku wakitumia malori yaliyowekwa namba bandia pamoja na nyaraka bandia ili kufanikisha wizi huo.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Temeke Giles Mroto akizungumza na wanahabari amesema watuhumiwa hao wamekamatwa baada ya kupata taarifa ya malori ya bidhaa za vifaa vya ujenzi na ngano vyenye thamani ya shilini milion 400 , ambayo yalichepushwa na watuhumiwa badala ya kupelekwa geita yalipelekwa mbeya na kufichwa.

Amesema watuhumiwa hao pia walibainika kuwa na mihuri,nyaraka bandia mbalimbali za ukaguzi wa mizigo lakini pia redio call ambapo baadhi yao walijifanya maafisa wa polisi katika kufanikisha wizi huo.

Aidha kutokana na kukithiri kwa wizi huo Kamanda mroto ametoa wito kwa wale wanaosafirisha mizigo ndani na nje ya nchi kwa kuwatumia madali au mawakala kuwa waangalifu.

Chanzo: Channel 10

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad