RC Gambo ameonya shule kugeuzwa kuwa matawi ya siasa


Mkuu wa mkoa wa ARUSHA,MRISHO GAMBO,ameonya shule kutogeuzwa kuwa matawi ya siasa na walimu wakuu kuacha kuruhusu hali hiyo na iwapo watabainika kukiuka agizo hilo watachukuliwa hatua za kisheria.


Gambo anatoa onyo hilo wakati akifungua mkutano mkuu wa mwaka wa wakuu wa shule za sekondari ARUSHA-TAHOSA-na kutoa angalizo kuwa shule ni eneo kwa ajili ya kutoa elimu kwa wanafunzi na si kitovu cha siasa.


Amesema kuna tabia imeanza kuibuka ya baadhi ya shule kugeuzwa vijiwe vya siasa na kuyataka mashirika yasiyo ya kiserikali endapo yanalengo la kusadia wanafunzi wanaopata mimba mashuleni ni vyema wakaweka mawakili wakuwaadhibu watu wanaowapa ujauzito wanafunzi.


Wakuu hao wa shule wametaja kuwa mkutano huo kuwa ni mojawapo ya jitihada mbalimbali wanazozifanya kuboresha elimu katika shule za sekondari mkoani ARUSHA.
Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad