Watu 16 Waaga Dunia Kwa Ajali ya Ndege

Watu 16 wamefariki kwenye ajali ya ndege ya jeshi la Marekani aina ya C-130 Hercules kwenye Jimbo la Mississipi nchini Marekani, ambayo imetokea katika eneo la LeFlore karibu kilomita 160 Kusini mwa mji mkuu wa jimbo hilo, Jackson.

Taarifa zimeeleza kuwa chanzo cha ajali hiyo ni mlipuko mkubwa uliotokea ndani ya ndege hiyo yenye injini nne.

Kwa mujibu wa jarida la Jimbo la Mississipi, ndege hiyo ilianguka katika shamba moja na mabaki yake yakatapakaa eneo hilo.

Aidha imeripotiwa kuwa miili ya marehemu 12 kati ya 16 wa ajali hiyo imepatikana katika eneo hilo ikiwa imeungua vibaya kwa moto.

C-130 Hercules ni ndege ya jeshi ambayo hutumika kusafirishia mizigo ya jeshi, kuzima moto na majanga ya aina mbalimbali.
Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad