Je Ali Kiba Tuendelee Kumuita King of Bongo Flava Au Tumpotezee...? Mwenye Afunguka Haya

Msanii wa muziki wa Bongo Fleva, Alikiba amesema atabaki kuwa mfalme wa muziki hapa Bongo ingawaje anaandamwa na watu aliokataa kuwataja moja moja.


Akitumia lugha ya mafumbo, Alikiba kupitia kurasa zake za mitandao ya kijamii ameoneshwa kukerwa na jambo hilo na kuamua kutema cheche huku akihoji kama walimpa kitanda basi waje wamtandikie alale kabisa.

“The KING ll always Be a KING. je Umeshakitandika nilale MALKIA wangu wa nguvu ??”,ameandika Alikiba pasi kujua ujumbe huo umemulenga nani.

Jana Tarehe 21 Agosti, Rapa Fid Q aliachia remix ya wimbo wake ‘Fresh’ ambao amewashirikisha Diamond Patnumz na Rayvanny, wimbo ambao mashairi ya Diamond yameonekana kuleta utata huku watu wengi wakihusisha kumlenga Alikiba.

  Moja ya mashairi hayo Diamond anasema “Ukinichukia sikosi hela hivyo kwangu sio kesi, Kunicompare na Cinderella haiwezi kuwa fresh” hapa swali linakuja Cindeella ni nani? bila shaka wote mnafahamu wimbo WA Cinderella uliomtoa Alikiba kwenye game.

 Na mashairi mengine ambayo yanahusishwa moja kwa moja na posti ya Alikiba ni pale Diamond Platnumz alivyosema “Si walitaka kiti, nimewapa hadi kitanda wakalale” kwani Alikiba nae ameonekana kukerwa na mistari hiyo na kujibu “je Umeshakitandika nilale MALKIA wangu wa nguvu?”.

Post a Comment

2 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.
  1. Ali kiba au nisema king kiba as he say will always be a king hata usemeje kwanza unajua mwanamke ndie mwenye tabia ya mafumbo isitoshe sijawahi kumsikia kiba kishindana sauti yake ya kipekee style zake A kipekee sasa wewe maskini ya mungu kinacho kushughulisha ni kipi unajipa majina wala hufanani be qho you are kumbukua uli kuwa wapi usiwe mwizi wa fadhila

    ReplyDelete
    Replies
    1. KING KIBA KASHAPOTEA SIZE YAKE SASA NI HAMONIZE ,DIAMOND ASIFANANISHWE NAVITU VYA AJABUAJABU KAMA ALIKIBA ,LEVEL ZA DIAMOND NI P SQUARE ,AKON,DAVIDO

      Delete

Top Post Ad

Below Post Ad