Masanja Hatimaye Baba Kijacho Mungu Ajibu Maombi


Masanja Hatimaye Baba Kijacho Mungu Ajibu Maombi
Wakati ndoa yake ikitimiza mwaka mmoja mwezi huu tangu ilipofungwa Agosti, mwaka jana ndani ya Kanisa la Mito ya Baraka lililopo Jangwani jijini Dar, aliyekuwa memba wa Kundi la Vichekesho la Orijino Komedi, Emmanuel Mgaya ‘Masanja Mkandamizaji’ huku masimango yakiwa mengi kutokana na kukaa muda mrefu bila mkewe, Monica kushika ujauzito, hatimaye Mungu amejibu maombi,

Chanzo makini kilicho karibu na staa huyo kililitonya  katika ndoa ya Masanja kulikuwa na changamoto kubwa kwani chokochoko na masimango vilikuwa vimeanza huku watu wakijiuliza kwa nini miezi yote hiyo mkewe hajapata ujauzito kwa sababu watu walishazoea mtu akiingia tu kwenye ndoa muda mfupi baadaye lazima ijibu.

“Kiukweli Masanja na Monica wamepitia kwenye masimango makubwa sana kwani watu walikuwa wakiwasimanga kwamba ndoa yao imechelewa sana kujibu huku wengine wakidai huenda kuna mkono wa mtu ndiyo maana wamekawia kiasi hicho
Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad