Nape Aguswa Zanzibar Kuvuliwa Uanachama CAF

Nape Aguswa  Zanzibar Kuvuliwa Uanachama CAF
Shirikisho la soka barani Afrika CAF lilitangaza kuivua Zanzibar uanachama wa CAF ikiwa ni miezi minne imepita toka shirikisho hilo liitangaze Zanzibar kuwa mwanachama kamili wa CAF.

CAF waliivua uanachama Zanzibar katika utawala wa Rais wa sasa wa CAF Ahmad Ahmad, baada ya utawala wa Rais  Issa Hayatoue kuondolewa katika nafasi hiyo na kurithiwa na Ahmad, moja kati ya sababu za Zanzibar kuvuliwa uanachama CAF wanadai hawaoni ulazima wa kuwa na wanachama wawili ndani ya taifa moja.

Waziri wa zamani wa habari, utamaduni, sanaa na michezo ambaye ni mbunge wa jimbo la Mtama kwa sasa Nape Nnauye ametumia ukurasa wake wa instagram kuandika mtazamo wake kuhusiana na kuvuliwa uanachama wa CAF na inavyomsikitisha.



“Jambo la Zanzibar kuonyang’anywa uanachama Wa CAF, nimejaribu kulielewa nimeshindwa! Jambo hili nililisimamia mpaka likawa baada ya kushindikana kwa miaka!kukubali kuondolewa kirahisi tu SI SAWA! Tena kwa fitina ya nchi moja! SI SAWA! Nashauri TUSIKUBALI KIRAHISI HIVI!”


Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad