Nchi ya Congo Imefungia Mitandao yote ya Kijamii


Serikali ya DR Congo imetoa amri ya kusitishwa kwa mitandao yote ya kijamii ili kuzuia usambazaji wa picha na video za ghasia zinzoendelea katika kanda hiyo .

Aidha hatua hiyo imechukuliwa kufuatia ongezeko la upinzani dhidi ya rais Joseph Kabila ambaye amekataa kujiondoa madarakani wakati awamu yake inamalizika mwezi Desemba .

Migomo ya kitaifa imepangwa kufanyika Jumanne na Jumatano .

Mapigano ya Jumatatu baina ya kundi la Bundu dia Kongo na vikosi vyaa usalama ,lilipelekea vifo vya watu 14 kutokea .

Mkuu wa idara ya mawasiliano nchini humo Oscar Manikunda Musata amefahamisha kwamba mitandao ya kijamii kama Twitter,Whatsap ,Facebook na Instagram itafungwa kwa muda .
Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad