Rais Magufuli Afuta Chaguzi Kata 25 Ndani ya CCM Baada ya Kuingiliwa na Makundi ya Wagombea Urais 2015

Mwenyekiti wa CCM, Rais John Magufuli, ameagiza kufutwa kwa chaguzi katika kata 25 nchini kutokana na dosari zilizotokea ikiwa pamoja na kuingiliwa na makundi ya wagombea urais wa mwaka 2015.

Akizungumza na waandishi wa habari leo jijini Dar es Salaam, Katibu wa Itikadi na uenezi wa chama hicho, Humphrey Polepole alisema pamoja na sababu hiyo, baadhi ya viongozi wa kata wameshindwa kutoa maelezo ya usimamizi wa mali za chama.

"Mwenyekiti wetu Rais Magufuli pamoja na Katibu Mkuu, Abdulrahman Kinana walipokea malalamiko ya wanachama na kuyatafakari na kuchukua hatua hiyo," alisema Polepole.
Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad