Awamu hii Mawaziri Wengi hasa Vijana Wamehamishia Ofisi zao Tweeter. Wanaondolea Stress Huko

Sijafahamu lakini nadhani kutakuwa na jambo. Kiuhalisia hakuna waziri anayesikika kwa sasa mpaka unaweza jiuliza waziri wa mambo ya ndani ni nani? unaweza jiuliza maswali hayo kwa wizara mbali mbali.
Wale vijana waliokuwa wakijitabanaisha kuwa ni wazalendo na wengine wakitaka kujitengenezea njia ya siku moja kuwa mabwana wakubwa wa nchi hii kwa awamu hii naona wengi ni kama wamelazimika kukalia mikia yao na kuinamisha pembe zao kama wanazo bado. wengine zilishakatwa kabisa.

 Mawaziri wengi wameishia kutoa stress zao na matamko Tweeter na Facebook huko utaona wanacho post utagundua wapo katika hali gani.

By Mtu Asiyejulikana

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad