Diamond Aamua Kumfuata Mama Watoto Wake 'Zari' Afrika Kusini

Diamond Aamua Kumfuata  Mama Watoto Wake 'Zari' Afrika Kusini
Ikiwa zimepita siku nne tangu mwanamuziki Diamond Platnumz akiri kumsaliti mpenzi wake Zari, hatimaye ametua nyumbani kwa mwanamke huyo nchini Afrika Kusini.

 Leo saa 5.40 asubuhi mwanamuziki huyo aliposti video katika mtandao inayomuonyesha akicheza na mtoto wake wa kwanza, Latifah huku kwa mbali ikisikika sauti ya Zari.

Dada wa mwanamuziki huyo, Esmah Khan aliposti video hiyo katika mtandao wa Instagram: “Tuko na Tiffah na mamy tunaita raha ya mtoto apewe mapenzi kwa baba na mama jamani.”

Leo ilikuwa siku muhimu kwa Zari kwani anasherehekea siku yake ya kuzaliwa.
Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad