Kichuya Aibuka Kidedea Mchezo wa Jana Dhidi Mbao

Kichuya Aibuka Kidedea Mchezo wa Jana Dhidi Mbao
Kiungo mahiri wa wekundu Msimbazi, Shiza Ramadhani Kichuya amechaguliwa kuwa mchezaji bora wa mechi iliyopigwa jana dhidi ya Mbao FC mchezo uliyopigwa katika viunga vya CCM Kirumba uliopo Jijini Mwanza.

Hayo yamewekwa wazi na taarifa iliyotolewa na ukurasa maalum wa Simba SC usiku wa kuamkia leo baada ya kiungo huyo kuisaidia timu yake kwa kuipatia bao la kwanza kwenye mchezo dhidi ya Mbao FC, katika mechi ya ufunguzi wa mzunguko wa nne katika michuano ya Ligi Kuu Tanzania Bara inayoendelea kutimua vumbi.

"Kiungo mahiri Shiza Kichuya amechaguliwa na wapenzi wa Simba kuwa mchezaji bora wa mechi dhidi ya Mbao FC. Shiza kichuya amekuwa akifanya vizuri katika nafasi ya kiungo mchezeshaji pia kweye safu ya ushambuliaji na hivyo kumfanya kuwa kiungo muhimu kwenye kikosi cha Simba", imesema taarifa hiyo.

Shiza Kichuya anakuwa mcheza wa pili kuchaguliwa na timu yake kuwa mchezaji bora tokea ilipoanza michuano ya Ligi Kuu Tanzania Bara.
Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad