Kubenea Atoa Siku Mbili Serikali Kulifungulia Gazeti la Mwanahalisi

Kubenea Aitaka Serikali Kulifungulia Gazeti la Mwanahalisi
WAHARIRI wa Gazeti la MwanaHalisi linalomilikiwa na Mbunge, Saed Kubenea lililofungiwa na serikali wamekanusha taarifa ya serikali kuwa gazeti hilo linaandika habari za uongo, wamedai kuwa wao hawajawahi kuandika uongo na badala yake huandika habari kwa weledi na ukweli.

Hayo wameyasema leo jijini Dar es Salaam wakati wakizungumza na wanahabari baada ya gazeti lao kufungiwa kwa muda wa miezi 24 (miaka miwili).

Aidha mmiliki wa Gazeti hilo, Saed Kubenea amesema kampuni yake Hali Halisi Publishers, imeiandikia barua Wizara ya Habari wakiitaka serikali kulifungulia Gazeti lao la MwanaHalisi ndani ya siku mbili (jana na leo), vinginevyo wataenda mahakamani kuidai serikali fidia ya Tsh. 141 Milioni kwa kila toleo.
Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad