MBUNGE Msukuma Afunguka Kuhusu Maiti iliyookotwa Mgodini GGM

Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi CCM, Geita, Joseph Msukuma ambaye pia ni Mbunge wa Geita Vijijini amemtaka Mkuu wa Mkoa wa Geita pamoja na Serikali ya Mkoa kufuatilia kwa karibu ripoti ya Uchunguzi wa mtu aliyekutwa amefariki ndani ya mgodi wa Dhahabu wa Geita.

Msukuma ametaka kufanyike uchunguzi wa kina kubaini chanzo cha vifo vya mara kwa mara vinavyotokea ndani ya Mgodi huo akisema kwamba hiyo sio mara ya kwanza kuokotwa maiti ndani ya GGM.

”Kumekuwa na matatizo yanayotokea kwenye mgodi mkubwa wa GGM. Niliwahi kuzungumza Bungeni kwamba kuna watu wanauawa katika mazingira ya kutatanisha lakini Jeshi la Polisi na Serikali ya Mkoa wa Geita haichukui hatua.

“Hali iliyotokea sasa, tarehe 18 imeokotwa maiti ndani ya Mgodi wakapewa watu kwenda kuzika lakini tarehe 23 mtu mwingine amefariki pale na amefariki katika mazingira ambayo wao walidai alitumbukia kwenye shimo – aliteleza kutoka juu.

“Tulipopata ile taarifa ilionesha ana majeraha kichwani ambayo hayalingani na maelezo kwamba ameporomoka kutoka juu.” – Mbunge Msukuma.
VIDEO:
Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad