Niki wa Pili Awatolea Uvivu Dogo Janja, Young Dee Awataka Washindane Kimuziki na Si Maisha Yao Binafsi

Niki wa Pili Awatolea Uvivu Dogo Janja, Young Dee Awataka Washindane Kimuziki na Si Maisha Yao Binafsi
Msanii kutoka kampuni ya Weusi, Nikki wa Pili ameingilia kati ugomvi wa Dogo Janja na Young Dee na kusema kwamba wanapaswa kushindana kimuziki na siyo kushambuliana katika maisha yao binafsi kwani jambo hilo linaweza kuja kuwaletea madhara kwa baadae

Nikki wa Pili amesema hayo kupitia kipindi cha eNewz kutoka EATV baada ya kupita siku kadhaa tokea Dogo Janja kutoa kauli yake ya kukataa kufananishwa na Young Dee kwa madai ni 'mteja wa unga' jambo ambalo lilizua makelele mengi kwa mashabiki wa wasanii hao pamoja na meneja wake Young Dee.

"Mimi naona kuna tatizo hapo, kwa sababu wameanza kuhusisha maisha yao binafsi, kwa hiyo ningefurahi kuona wanashindana kimuziki zaidi. Maana unapokuwa maarufu ukiongea kitu ujue kinaishi kwa kipindi kirefu na hakiwezi kufutika kiurahisi, kwa hiyo ni vizuri kuchagua maneno ya kutumia", amesema Nikki wa Pili.

Mtazame hapa Nikki wa Pili akifunguka mengine zaidi kuhusu ugomvi baina ya Dongo Janja na Young Dee

Post a Comment

1 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.
  1. Hawana lolote wanatafuta Kiki tu na hayo mambo yeshapitwa na wakati

    ReplyDelete

Top Post Ad

Below Post Ad